MBUNGE wa Kawe Bi. Halima Mdee (CHADEMA) pamoja na Mbunge wa Viti Maalum Bi. Ester Bulaya (CCM) wameamua kujitokeza kumsaidia msanii Elizabeth Michael ‘Lulu’ anayetuhumiwa kumuua aliyekuwa mwigizaji marehemu Steven Kanumba.
Wabunge hao juzi waliamua
kwenda kumuona Lulu na kwa sasa
wameamua kuendesha kampeni ya
kuchangisha fedha za malazi kwa
ajili ya familia yake.
Bi. Mdee kupitia ukurasa wake wa
mtandao wa kijamii Twitter alisema
Lulu anahitaji mwanasheria makini
wa kuweza kumnasua kwenye kesi
hiyo akiwemo Mwanasaikolojia wa
kuzungumza naye ili aweze kuwa
vizuri kiakili.
Mbunge huyo wa Jimbo la Kawe
aliandika katika ukurasa huo kuwa
“Leo (mwishoni mwa wiki) mimi
na Mheshimiwa Bulaya tulikwenda
kumuona Lulu Oysterbay Polisi.
‘She really needs our support’ (
kwa kweli anahitaji msaada wetu).
Kwanza ‘she is only 17’ (kwanza
huyu ni binti wa miaka 17 tu).
“Pili anahitaji sana psychological
support (msaada wa kisaikolojia).
Nawaomba watu wenye taaluma
hiyo wasisite kwenda kumuona.
Wasiliana na 0714282527 Steve
Nyerere. Tatu anahitaji wanasheria
makini wa kumsaidia na kwa
yeyote ambaye yuko tayari naomba
awasiliane nami 0759 569823
(Halima Mdee). Nne, at that
tender age (kwa umri huo Lulu)
ndio alikuwa anategemewa na
familia yake. Now (sasa) yuko
ndani matatizo yamezidi kuwa
makubwa.
“Kwa yeyote anayeguswa,
naomba atume chochote kwenye
namba hii 0754 878890 ni namba
ya M-Pesa ya mama yake tumsaidie
huyu mtoto!...”Again (tena)..
namba ya M-PESA kwa wanaotaka
kumsaidia Binti yetu Lulu ni
+255754878890. Ni namba ya
mama yake,” aliongeza Bi.Mdee.
0 comments:
Post a Comment